Advertisements

Friday, August 11, 2017

Serikali kuja na mashahidi 10 kesi ya dawa za kulevya inayomkabili Manji

Serikali imeieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwamba itafika na mashahidi wasiozidi 10 katika kesi ya kutumia na kujihusisha na dawa za kulevya inayomkabili mfanyabiashara, Yussuf Manji.
Hayo yameelezwa na Wakili wa Serikali Mkuu, Timony Vitalis mbele ya Hakimu Mfawidhi, Cyprian Mkeha baada ya kumsomea Manji maelezo ya awali (Ph) ambapo katika maelezo hayo, Vitalis amedai mshtakiwa ni mkazi wa Sea view DSM, pia ni mfanyabiashara anayetuhumiwa kujihusisha na kutumia dawa za kulevya.
Amedai kuwa alikamatwa February 2, 2017 kisha akapelekwa kituo cha Polisi ambapo alichukuliwa hadi nyumbani kwake na kupekuliwa na baada ya kupekuliwa alipelekwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali na kuchukuliwa haja ndogo (Mkojo) ambao ulipimwa na kukutwa na dawa za kulevya aina ya Benzodiazepine.
Baada ya kusomewa maelezo hayo, Manji alikubali wasifu wake kwamba ni mfanyabiashara, makazi na jina lake licha ya kudai limekosewa ila usahihi ni Yusuf Manji huku akikana maelezo mengine.
Aidha, wakili Vitalis ameieleza Mahakama kwamba wanaomba kupangiwa tarehe kwa ajili ya kesi hiyo kuanza kusikilizwa, pia wanatarajia kuwa na mashahidi wasiozidi 10 hivyo Hakimu Mkeha ameahirisha kesi hiyo hadi August 22, 23, na 24, 2017 kwa ajili ya kusililizwa mfululizo.

No comments: